ZBS yachangia kambi ya matibabu ya ZMBF

NA MWANDISHI WETU

TAASISI ya Viwango Zanzibar (ZBS) imeeleza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali ili kuimarisha ustawi wa jamii na uchumi kupitia njia mbali mbali.


Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Yusuph Majid Nassor, alieleza hayo jana wakati akikabidhi msaada wa vifaa vya uchunguzi na matibabu kwa taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) kwa ajili ya kambi ya uchunguzi wa afya na matibabua itakayofanyika kuanzia Septemba 30 hadi Oktoba 2, mwaka huu.

Yusuph alieleza kuwa hatua hiyo inaangukia katika moja ya maeneo yanayosaidiwa na taasisi yake kupitia mpango wa kusaidia jamii na wadau wake ikiwemo taasisi hiyo ambayo ni miongoni mwa wateja wake.

“Kila mwaka huwa tunatoa sehemu ya mapato tunayokusanya kwa jamii na tumelkua tukipeleka msaada kwa wizara ya afya na kwa mwaka huu tunaelekeza sehemu ya mapato hayo katika tukio hili kuiunga mkono ZMBF lakini pia wizara ya afya”, alieleza Yussuph.

Hata hivyo aliahidi kuwa taasisi yake itaendelea kusaidia shughuli za taasisi hiyo kupitia mpango wa kuimarisha shughuli za ujasiriamali na kuishauri ZMBF kufanya kazi kwa karibu na taasisi hiyo ili kuwasaidia wajasiriamali hasa wadogo.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya mwenyekiti wa bodi ya ZMBF, Mama Mariam Mwinyi, Ofisa Mterndaji Mkuu wa Zanzibar Maisha Bora Foundation, Fatma Fungo, mbali ya kuishukuru ZBS, alieleza kuwa msaada huo umekuja wajkati muafaka na kwamba utasaidia katika kambi hgiyoo itakayofanyika Dole, wilaya ya Magharibi ‘A’, Unguja.

Alieleza kuwa kambi hiyo itatanguliwa na matembezi ya kilomita tano yaliyolenga kujenga tabia ya watu kupenda kufanya mazoezi kama sehemu ya mkakati ya kulinda afya na uchunguzi wa maradhi mbali mbali pamoja na matibabu.

“Mtakumbuka mama Mariam (mke wa Rais wa Zanzibar) kila mwezi alikua na matembezi yalilenga kuimarisha afya za wananchi ikiwa ni miongoni mwa malengo ta taasisi yetu lakini sasa matembezi yale tumeyaimarisha na tutayazindua rasmi Septemba 30, pamoja na kampeni ya ‘Afya bora, Maisha bora’”, alieleza Fatma.

Aliongeza kuwa katika kambi hiyo wanatarajia kuwaona zaidi ya watu 3,000 ambao watafanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu ya magonjwa mbali mbali ikiwemo chanjo ya ugonjwa wa UVIKO 19, kisukari na shinikizo la damu (presha).

Hata hivyo alitoa wito kwa wadau kuendelea kuchangia kambi hiyo itakayoendeshwa na madaktari kutoka ndani na nje ya Zanzibar chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya na wananchi kujitokeza katika matembezi hayo yanayotarajiwa kuanzia katika ofisi za Manispaa ya Magharibi ‘A’, Kianga.

Kwa mujibu wa ZMBF matembezi hayo yaliyopewa jina la ‘Mariam Mwinyi Walkathon’ yanatarajiwa kuongozwa na mama Mariam Mwinyi atakayeambatana na viongozi mbali mbali wa serikali, vyama vya siasa, vikundi vya mazoezi, wajasiriamali na vikosi vya ulinzi na usalama ambapo pia kutakua na uchangiaji wa damu.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango