Msaada wa kisheria unahitajika kuwaokoa watoto wanaokinzana na sheria
NA AMINA MCHEZO
MSAADA wa watoto kisheria, kisera na kimipango ni uwanja mpana huku ikionekana sheria iliopo Sasa ya mtoto sheria namba 6 ya mwaka 2011 inamapungufu hivyo wizara ya Màendeleo ya jamií, jinsia, wazee na watoto Zanzibar inafanya juhudi kuhakikisha sheria hiyo inapitiwa upya.
"Kwa Sasa tumeshatoka kwenye
hatua nyingi za ukusanyaji wa maoni ya wadau na Sasa nadhani tupo katika hatua
ya kuishirikisha tume ya marekebisho ya sheria ili tuone kwamba tunapata baraka
za mwisho na kunipeleka mbele ili tuwe na sheria mpya ili mambo yawe mazur Kwa
watoto" Amesema mkuu wa wa Division
ya hifadhi ya mtoto kupitia idara ya ustawi wa jamii na wazee.
WASAIDIZI wa Sheria (Paralegal) wakiwa katika moja ya mikutano ya kujengewa uwezo ili watoe huduma bora wa wateja wao.
Mtoto anaekinzana na sheria ni
mtoto yeyote alie chini ya umri wa miaka 18 ambae amefanya makosa ya kijinai
ikiwemo kubaka, kulawiti, wizi na makosa mengine.
Utafiti umebaini kuwa watoto wengi
wanaokinzana na Sheria ni wale watoto wa mzazi mmoja, ndoa kuvunjika, Kukosa
matunzo Kwa wazazi wake, hivyo watoto hao hupelekea kuathirika kiakili Kwa
kujiingiza katika makundi maovu na
kufanya makosa ya kijinai.
Kiuhalisia kutokana na sababu hizo
inaonekana wazi watoto wanaokinzana na sheria wengi wao ni wale waliopitia
udhalilishaji Kwa namna Moja au nyengine kutokana na Kukosa malezi sahihi na
Kukosa haki zake za msingi kama mtoto.
Msaada wa kisheria Kwa watoto
wanaokinzana na sheria umeibua hisia tofauti Kwa wanajamii hasa pale wanapoona
makosa ya namna hiyo yakijirudia Kila mara.
MMOJA ya watoa maada wa kisheria akikabidhiwa cheti baada ya mafunzo yaliyotolewa na Idara ya Msaada wa Kisheria Zanzibar.
Wengine wanasema kupatiwa msaada wa
kisheria ni sawa tu kwani wale ni watoto mengi wanayafanya Kwa kutokujua.
Huku mitazamo ya wengine
yakionekana kubeba hisia Kali na kukataa kabisa watoto wale kupewa msaada
wakidai kuwa ni njia Moja ya watoto hao kuendelea kutenda makosa Kila siku.
"Sioni sababu ya watoto
wanaotenda makosa kupewa msaada wa kisheria
kwani nao wanajielewa na wakisaidiwa
kisheria yaani watoto watakuwa wanajiamini Sana", wamesema baadhi
yao.
Mtumwa Ameir Ali Msaidizi wa Sheria
(Paralegal) kutoka wilaya ya Mjini amesema bado baadhi ya wanajamii hawajaelewa kuhusu kutolewa Kwa
msaada wa kisheria Kwa watoto wanaokinzana na sheria.
Amesema ushawishi wao ni mkubwa Kwa kutafuta wakili wa usimamizi wa kesi za watoto pamoja na wao kumpa elimu na ushauri ili asirudie tena kosa lile.
Amefahamisha kuwa kumuacha mtoto
aliekinzana na sheria ni kumkosesha haki zake za msingi ikiwemo kusoma pindi tu
atakapokaa chuo Cha mafunzo Kwa Kukosa usaidizi wa kisheria.
"Baadhi ya wajamii hawana
uwelewa Kwa sababu wanaona yule mtoto ameshatenda Lile kosa kwanini sisi
tunakaa tunamtetea lakini jamii hawajui kuwa Lile kosa linaweza kuwa lisiwe
lake au amefanya kosa Kwa ule utoto tu." amesema.
Mtumwa amesema japokuwa sheria haiwaruhusu
kusimamia mashauri mahakamani lakini hawawezi kumuacha mtoto aliekinzana na
sheria hivyo wanaanza ngazi za awali ikiwemo polisi ili apate haki yake Kwa
wepesi na haraka.
Kwa mujibu wa kitengo cha takwimu Dawati
la Jinsia Makao Makuu ya polisi Zanzibar kuna kesi 129 zilizoripotiwa na
kufikishwa katika mahakama tofauti Zanzibar katika kipindi cha kuanzia Januari
Hadi November 2023 zinazowahusu watoto waliokinzana na sheria .
Ripoti hizo zinaonesha kwamba, kesi
70 ni za mkoa wa Mjini Magharibi, 8 mkoa wa Kusini Unguja, 21 mkoa wa Kaskazini
Unguja, 16 mkoa wa kusini Pemba na kesi 14 ziliroipotiwa mkoa wa Kaskazini Pemba.
Akizungumza na mwandishi wa makala
hii, Mratibu wa Dawati la jinsia Makao
Makuu ya Polisi Zanzibar, Sajenti Rahma Ali Salum, amesema watoto wanaokinzana
na sheria wanawaangalia kama watoto wengine hasa katika kuwasaidia kwa kuwapatia
elimu ya kujitambua.
Amesema katika usaidizi wao wa kisheria kwa watoto wa
namna hii wanashirikiana na wasaidizi wa sheria, waratibu wa shehia pamoja na
ustawi wa jamii Kwa kusikiliza kesi zao Kwa pamoja.
Sajenti Rahma amefahamisha kuwa ni
wajibu wa watoto wanaokinzana na sheria kupatiwa msaada kutokana na mazingira
yanayojitokeza wakati wanapofanya makosa.
"Tukifuatilia kesi zao nyingi
ni ushawishi wa watoto wezao, wengine kuwa na njaa kutokana na Kukosa chakula
nyumbani ilimradi makosa yao mengi ni ya ushawishitu", amesema Sajenti
Rahma.
Ameongeza kuwa Dawati la jinsia
wanapopokea kesi za watoto waliotenda makosa wanawaita wazazi wao kuwafahamisha
namna ya kukaa na mtoto wake kwani wazazi wengi huwachukia watoto wao kutokana
na makosa yao.
"Msaada wa kisheria sana
wanapewa na Wasaidizi wa Sheria wanaokuwa pamoja na wazazi wao, sisi
tunawafahamisha namna yale makosa yalivyo na mtoto akaenae vipi kwa sababu
wazazi wengine wanakua wakali na kuwachukia", amesema.
Amefahamisha kuwa katika kuwasaidia
watoto wamekuwa wakipelekwa katika mahakama ya watoto ili wapate uhuru wa
kujieleza mbele ya mahakama.
Jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar
ZAFELA ni jumuiya isiyo ya kiserikali ambayo inatoa msaada wa kisheria Kwa
wanawake na watoto imesema Kuanzia January Hadi November 2023 jumla ya kesi 11
za watoto wanaokinzana na sheria
zimefika ofisini kwao na wameanza
kuzishughulikia Kwa kuwapatia msaada wa kisheria na kesi 3 tayar
zimeshapatiwa ufumbuzi Kwa kutozwa faini.
Mwanaisha Mustapha ni Mwanasheria
kutoka Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA)amesema kwa watoto
wanaokinzana na sheria wamekuwa wakiwasimamia kwa hali ya juu kwani wengi wao
makosa yao ni ya kusingiziwa au ya kulipiziwa visasi Kwa baadhi ya wanajamii
waliomzunguka.
Amesema wao kama wanasheria
wanasimama kwenye sheria ya mtoto inavyozungumza katika kumlinda kama mtoto
mwengine mpaka pale mahakama itakapomtia hatiani Kwa kosa Lile.
Amefahamisha kuwa hali ya sasa asilimia
kubwa watoto kwa watoto wanafanyiana udhalilishaji jambo ambalo wanataasisi
zinazotoa msaada wa kisheria wamekuwa macho ili
jamii ibaki kuwa salama.
"Ni janga kubwa hali ya
udhalilishaji na hali ya sasa hivi iliokuwepo asilimia kubwa watoto Kwa watoto
ndio wengi ambao wanafanya haya matukio Kwa iyo tukiwaangali kisheria wote ni
watoto na wote wanataka kulindwa na sheria", amesema Mwanaisha.
Aidha Wakili Jamila Massoud kutoka Shirika
la Msaada wa Kisheria nà Haki za Binaadam
Zanzibar (ZALHO) amesema wanashuhulikia kesi 19 huku 7 kati yao zikiwa
zimeshafikishwa mahakamani Vuga zinazowahusu watoto wanaokinzana na sheria.
Amesema shirika limekuwa na
utaratibu wa kuandaa mikutano na wanajamii ili kuzungumza nao na kuwafahamisha kwanini
watoto waliokinzana na sheria wanatakiwa kupatiwa msaada wa kisheria.
Amebainisha kuwa pale
wanaposhughulikia kesi za watoto wanaokinzana na sheria wanashauri Sana
kubadilishiwa makaazi pale anapokuwa tayar ameshakuwa mtoto mwema kwenye jamii
ili asirudia tena makosa yale.
"Tunawapa muelekeo au tunawapa
utaalamu kwanini tunawasaidia hawa watoto Kwa sababu hawa ni Victim wa
udhalilishaji ukiangalia mtoto anaekinzana na sheria utagundua kuwa nae kadhalilishwa
Kwa namna Moja au nyengine", amesema wakili huyo.
Mohammed Khamis Faki, mkaazi wa
Kazole anaemlea mtoto wa dada yake
ajulikanae Kwa jina Khamis Mwadini Kheir mwenye umri wa miaka 16 alishtumiwa Kwa kosa la kukashifu
mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 mnamo mwezi wa march 2023 huko maeneo ya
Daraja bovu wilaya ya maghari A unguja.
Katika shitaka hilo lililopekea
kufikishwa kituo Cha polisi Mwera na kesi kupelekwa mahakamani Vuga mjini
unguja, ndugu Mohd Khamis amesema baada ya kufikishwa mahakamani shtaka la
mjomba wake awali walishindwa Kwa Kukosa wakili kutokana na hali yao ya
kimaisha.
"Tulipandishwa mahakamani Vuga
tulishindwa kupata wakili kutokana na hali zetu ndipo tukaunganishwa na Mtu
kwenye hili shirika hili pale mikunguni linalosaidia watu wasio na uwezo na Kwa
uwezo wa Mwenyezi Mungu Lile shirika lilitusaidia mpaka kesi ilipomalizika na
alhamdullillah hatukutozwa ushuru wowote
ule", ameongeza
Amesema msaada walioupata kutoka
shirika la ZALHO ni mkubwa kwani walishindwa na fedha za kuwapa wakili ili
kuwasaidia kesi ya mjomba wake na Kwa Sasa mjomba wake huyo yupo huru na
amejifunza kutokana na kosa Lile pamoja na kimkataza kufika katika mtaa
aliopatia mtihani huo.
"Kwa Sasa tumempiga Marufuku
kufika mitaa ya Daraja bovu ambako ndipo alipo huyo binty kwenye hiyo nyumba
aliofika mjomba wangu na kwa sasa hata hasogei kwani ulikuwa ni mtihani tu ule kwake"
Amesema.
Wizara ya Màendeleo ya Jamií,
Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar imesema hali ya upatikanaji huduma kisheria Kwa
watoto ni ndogo na ndio maana wameona Kuna haja ya kutia mkono sheria iliopo
Sasa ili kuboreshwa Kwa huduma.
Mkuu wa Division ya hifadhi ya
mtoto katika Idara ya Ustawi wa Jamii na Wazee, Sheikh Ali Sheikh amesema
watoto wanaokizana na sheria sheria bado inamtanzama kama mtoto mbali ya kuwa
wanatenda makosa lakini sheria inataka kuwalinda pia na kupewa haki zao.
Amesema kama idara inatoa msaada wa
kisheria Kwa kuwasimamia mahakamani hadi pale hukumu zinapotokea ambazo
kikawaida ni kutozwa faini tu na sio kufungwa baadae idara inawapeleka vituo
vya kurekebisha tabia kwenda kupata ujunzi na kujiweka sawa.
"Tunamsaidia kama mtoto kama
sheria inavyotaka atizamwe Kwa hiyo Kuna maafisa wetu mahakamani kuhakikisha
juu ya kesi zao kama watenda makosa lakini mwisho wa siku Sheria inataka
iwalinde" amesema.
Kwa mujibu wa Wizara taasisi za
usaidizi wa sheria, waratibu na wadau mbali mbali mbali, suala la usaidizi wa
sheria linahitaji kupewa kipaumbele Zaid huku wazazi nao wakitakiwa kusimamia
msingi mzima wa malezi Kwa watoto wao ili kupatikana kizazi chenye maadili
mazuri.
Comments
Post a Comment