Wanahabari wanawake wapewa mbinu kukwepa udhalilishaji mitandaoni


NA AMINA MCHEZO

WAANDISHI wa habari wanawake wananafasi na mchango mkubwa katika kuielimisha jamii kupitia mitandao ya kijamii kukizingatiwa usalama wao.

Akifungua mafunzo ya siku mbili  kwa waandishi wa habari wanawake Zanzibar, Mkufunzi na mwanahabari mkongwe kutoka nchini Kenya,  Cecilian Maundu (pichani), amesema wanahabari wanawake wamekuwa wakipitia wakati mgumu wakiwasilisha kazi zao za kimtandao ukilinganisha na wanahabari wa kiume.

Amesema hali hiyo huwawia vigumu baadhi ya waandishi kuendelea na kazi yao na wengine kuathirika kisaikolojia kutokana na baadhi ya wafuasi wa kimtandao kuwatolea maneno ya kashfa pasi na wao kuridhia.

Maundu amesema hali hiyo inaweza ikaondoka au kusaidiwa endapo kutakuwa na ushirikiano wa pamoja kati ya waandishi na taasisi za kihabar ili kuunda kikosi kazi ambacho kitamlinda mwandishi pale tu anapopata kadhia ya kimtandao.

"Zanzibar mnapaswa kutumia taasisi hizi kama ZPC, TAMWA, MCT na nyengine ili pale kuona mnashambulia Kwa pamoja mitandaoni kukomesha udhalilishaji huu", ameongeza Cecilian.

Hata hivyo amewatahadharisha wanahabar wanawake kuacha  kuweka taarifa zao binafsi mitandaoni kwani baadhi ya wakati huwageukia na kutumika katika udhalilishaji.

"Kama mwanahabar anataka kuweka taarifa zake binafsi basi lazima azifiche na aweke neno la Siri (password) ambayo watu hawataweza kuingia la si hivyo taarifa hizo mwisho wake huwa mwiba kwake", ameongeza.

Wakichangia wakati wa mafunzo hayo, baadhi ya waandishi walioshiriki mafunzo hayo Najjat Omar kutoka The Chanzo online na Khairat Haji kutoka Chama cha  Waandishi wa Habar Wanawake Tanzania (TAMWA ZANZIBAR) wamesema hali bado ni mbaya kwa waandishi wanawake pale wanapowasilisha kazi zao mitandaoni kutokana na kukosa msaada kwenye taasisi husika.

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyobeba ujumbe wa ‘Namna ya kuwa salama mtandaoni’ yamedhaminiwa na shirika la Pen America la nchini Marekani.

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango