NBC yazindua kampeni ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako’ kukuza uchumi wa wateja wake

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua kampeni mpya ya akiba inayolenga kuunga mkono juhudi za serikali za kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kidigitali zinazotolewa na taasisi za kifedha nchini.

Kampeni hiyo ya ‘Shinda Mechi Zako Kinamna Yako’ inawahusu wateja binafsi, waajiriwa, wamiliki wa biashara ndogo na wanafunzi ambayo itaambatana na  zawadi mbali mbali ikiwemo ya gari mbili aina ya BMW x1.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es salaam jana, Mkuu wa kitengo cha masoko wa benki hiyo, David Raymond, alieleza kuwa mpango huo unalenga kuimarisha ustawi wa kifedha miongoni mwa wateja wa benki hiyo na kuchochea ukuaji wa uchumi jumuishi kupitia huduma rasmi za kifedha.

“Tunanalenga kuitumia falsafa ya mchezo wa soka ambao benki ya NBC ni Wadhamini wakuu wa ligi tatu. Tunapoingiza falsafa hiyo kwenye maisha ni wazi tunatambua wateja wetu wana ndoto, malengo na maazimio katika kufanikisha maendeleo yao kiuchumi yakiwemo ya ujenzi, kukuza biashara, kusomesha watoto na mengine mengi”, aalieleza Raymond.

Aliongeza kuwa mkakati huo unahusisha agenda ya kutoa elimu kwa wananchi na kuwashawishi watumie huduma rasmi za kibenki zinazogusa rika na makundi yote ya kijamii na kutaja huduma zinazohusishwa na kampeni hiyo kuwa ni pamoja na akaunti ya Chanua ambayo ni mahususi kwa watoto, Malengo, Akaunti ya Johari mahususi kwa wanawake na akaunti ya Mwalimu.

Alitaja akaunti nyengine kuwa ni ya mshahara, akauti ya wajasiriamali, akaunti ya wanafunzi, akaunti ya kua nasi, akaunti ya vikundi, akaunti binafsi na akaunti ya biashara.

Akizungumzia zawadi zinazotolewa kupitia kampeni hiyo, Meneja Bidhaa na Mauzo, Dorothea Mabonye, alisema itadumu kwa mwaka mmoja inahusisha zawadi za kila mwezi na mwisho wa mwaka ikiwemo zawadi kuu ya gari aina BMW X1.

Alieleza kuwa zawadi hizo zitakazotolewa kwa washindi wawili, fedha taslimu, zawadi ya safari ya mapumziko nchini Singapore, simu za mikononi, komyuta mpakato (laptops), friji, ‘tablets’ za watoto pamoja na majiko ya kisasa ya kupikia.

Mmoja wa mabalozi wa kampeni hiyo, Nasry Ramadhani ‘Ujugu’ ambae ni mjasiriamali aliyewekeza kwenye biashara ya kuonesha burudani ya mpira kupitia TV jijini Dar es salaam, aliwasihi wajasiriamali wakiwemo vijana kutumia vema fursa hiyo iliyotolewa na benki ya NBC kupitia kampeni hiyo ili waweze kunufaika kupitia faida mbalimbali zitokanazo na matumizi ya huduma rasmi za kifedha.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango