Watoa huduma 100, wanafunzi 500 wa Muhimbili wapatiwa chanjo homa ya ini
#KaziInaongea
SERIKALI ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais, Dk. Samia Suluhu
Hassan, kupitia Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, hivi karibuni imefanya vipimo
na kutoa chanjo ya Homa ya Ini kwa watoa huduma za afya 100 wa Kitengo cha
dharura Hospitali ya Taifa Muhimbili na
wanafunzi 500 wa Chuo cha Sayansi
Muhimbili (MUHAS).
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amesema kuwa, Muhimbili kwa kushirikiana
na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), wamezindua
mpango wa kuwapatia chanjo dhidi ya Virusi vinavyosababisha Homa ya Ini
(Hepatitis B Vaccine) kwa wafanyakazi hao na wanafunzi Chuo Kikuu cha Afya cha
Muhimbili (MUHAS).
“Leo nimeshiriki uzinduzi wa
zoezi la upimaji na chanjo ya homa ya Ini kwa watoa huduma za afya kitengo cha
dharura Hospitali ya Taifa Muhimbili na wanafunzi wa Chuo cha Sayansi
Muhimbili”, amesema Prof. Janabi.
Amefafanua kuwa, chanjo hii ni
muhimu sana kwa watoa huduma za afya ambao wako kwenye hatari mara 10 zaidi ya
kupata maambukizi ya Homa ya Ini ikilinganishwa na watu wa kawaida.
Kwa mujibu wa WHO, mwaka 2022,
zaidi ya watu Milioni 254 walikuwa wakiishi na maambukizi sugu ya Homa ya Ini,
na zaidi ya watu Milioni moja walifariki kutokana na magonjwa yanayohusiana
nayo kama saratani ya ini.
Aidha Dk. Janabi amewasihi
wananchi kuchukua hatua sasa ya kujikinga na ugonjwa huo kwa kupata chanjo,
ambayo ni salama, bora na rahisi kupatikana.
Comments
Post a Comment