Posts

Showing posts from April, 2025

Takribani watu 50 hufariki kwa maradhi ya moyo duniani kila siku

Image
NA   MWANDISHI MAALUMU , ZANZIBAR IMEELEZWA kuwa ma radhi  ya moyo na shinikizo la damu yana changia takribani vifo vya watu milioni 20 kwa mwaka u limwengu ni, idadi ambayo ni sawa na   vifo 50 k w a siku. Akifungua mkutano wa tatu wa kimataifa wa maradhi ya moyo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , D kt . Samia Suluhu Hassan , Makamu wa Pili wa Rais wa  Zanzibar , Hemed Suleiman Abdull a, a lieleza kuwa k wa Ta nzania takribani  watu milioni 4.9 wanas umbuliwa na magonjwa hayo amba yo huchangia asilimia 13 ya vifo v inav yote kea  nchini. Hivyo aliwa himiza washiriki wa mkutano huo kutumia fursa waliyoipata kujumuika pamoja kutafuta mbinu za kudhibiti ongezeko la magonjwa h ayo  kwa   kujengeana uwezo na ku imarisha nyenzo za utendaji kazi ili kukabiliana na tabia zinazochochea  magonjwa yasioyoambukiza h ususani ya  moyo na mishipa ya damu . MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kis...

ZBS kuifanya Z'bar kitivo cha maabara Afrika

Image
NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS), Yussuph Majid Nassor, amesema kuwa taasissi hiyo inatarajia kujenga maabara kubwa katika eneo la uwekezaji wa viwanda liliopo Dunga Zuzeitakayokuwa kitivo cha maabara Afrika. MKUU wa usalama wa bandari ya Fumba, Juma Ali (kulia) akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea bandari hiyo kukagua kazi za taasisi ya viwango Zanzibar (ZBS) ikiwa ni sehemu ya Jukwaa la Viwango 2025 lililoandaliwa na ZBS. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya ZBS, Balozi Omar Yussuf Mzee, ktikati ni mkurugenzi mkuu wa ZBS, Yussuf majid Nassor.  Majid alieleza hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake Maruhubi baada ya waandishi na watendaji wa taasisi hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Balozi Omar Yussuf Mzee, kutembelea maabara mbali mbali za taasisi hiyo na bandari za fumba na bandari kavu ya maruhubi kuangalia namna taasisi hiyo inavyofanya kazi. Ziara na mazungumzo hayo ni sehem...

ZEC yataka mijadala ya uchaguzi ihusishe wataalamu wa uchaguzi

Image
NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR    MKURUGENZI  wa uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous Faina, amesema kuwa kuitisha mijadala inayohusiana na uchaguzi kwenye vyombo vya habari bila ya kuwepo wataalamu wa tume ni kosa kisheria. Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki visiwani hapa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) katika mkutano mkuu na mafunzo yaliyodhaminiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Mashirika yay Umma (PSSSF). Alisema kuna baadhi ya vyombo vya habari vinaendesha mijadala kwa kuhusisha watu wasiokua na majibu sahihi kuhusu uchaguzi na kuwaweka njia panda jambo ambalo ni kinyume na sheria. Aidha alivitaka vyombo vya habari vinavyotaka kuendesha mijadala kuhusu uchaguzi ni vyema kuwasiliana na Tume ya Uchaguzi ili vipatiwe maafisa watakaotoa majibu sahihi kwa masuala yatakayoulizwa. "Hii ni rai kwenu nyinyi waandishi wa habari ni busara zaidi kama kuna mijadala inaendeshwa katika vyombo v...