ZBS kuifanya Z'bar kitivo cha maabara Afrika
NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR
MKURUGENZI Mkuu wa
Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS), Yussuph Majid Nassor, amesema kuwa taasissi hiyo inatarajia kujenga
maabara kubwa katika eneo la uwekezaji wa viwanda liliopo Dunga Zuzeitakayokuwa kitivo
cha maabara Afrika.
Majid alieleza hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake Maruhubi baada ya waandishi na watendaji wa taasisi hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Balozi Omar Yussuf Mzee, kutembelea maabara mbali mbali za taasisi hiyo na bandari za fumba na bandari kavu ya maruhubi kuangalia namna taasisi hiyo inavyofanya kazi.
Ziara na mazungumzo hayo ni sehemu ya Jukwaa la Viwango linaloandaliwa na taasisi hiyo kila mwaka na kuratibiwa na Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) ambapo Majid alieleza kuwa ujenzi wa maabara hizo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 36 kutoka sasa.
Alifafanua kuwa kukamilika kwa ujenzi huo kutaitangaza Zanzibar na kuwa kitivo cha maabara katika ukanda wa Afrika mashariki na kati hivyo kukuza na kuimarisha biashara kati ya Zanzibar na maeneo mengine ulimwenguni.
Alisema tasnia ya ujenzi Zanzibar imekuwa kubwa na ndio maana wanajenga maabara nyingi na tayari wamejenga maabara kubwa ya vifaa vya ujenzi ili vifaa hivyo vipimwe Zanzibar.
Alisema
awali wawekezaji walikuwa wakipeleka vifaa vyao vya ujenzi Tanzania bara kwa
ajili ya kupima ubora.
AFISA Uhandisi ujenzi wa maabara ya ujenzi za ZBS, Salim Kassim Juma (kushoto), akitoa maelezo waandishi wa habari kuhusu ufanyaji kazi wa maabara hizo wakati wa ziara ya waandishi wa habari.
Alisema ZBS ilianza na maabara nne lakini kwa sasa inamaabara 10 na ndani ya miezi minne ijayo itakua na maabara 13 ili kukidhi kiu ya uingiaji wa mizigo Zanzibar na kumlinda mtumiaji wa mwisho.
Alisema bado kuna changamoto ya upimaji ubora wa vifaa kisiwani Pemba ambapo vifaa hutoka Pemba na kupimwa Unguja hivyo pia serikali inatarajia kujenga maabara kisiwani humo.
Alisema serikali imejikita katika maabara ya uchumi ya buluu ambapo, watapima viwango vya ubora wa uvuvi ikiwemo samaki, dagaa, mwani, gesi na mafuta.
Naye
Mwenyekiti wa Bodi ya ZBS, Balozi Omar Yussuf Mzee, alisema kazi ya kuelimisha
taifa sio kazi ndogo hivyo aliwapongeza waandishi wa habari kwa kazi kubwa
wanayoifanya.
Alisema
waandishi wa habari wana umuhimu mkubwa kwa ZBS kwasababu lengo la uwepo wa
taasisi ni kumlinda mlaji kwa kuhakikisha bidhaa zinazoingiza zinakuwa na
ubora.
Comments
Post a Comment