NBC yaahidi makubwa ligi kuu Tanzania bara

NA MWANDISHI WETU

MDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jana ilikabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya soka ya NBC (NBCPL) kwa timu ya Yanga SC ya jijini Dar es Salaam iliyoibuka bingwa wa kombe hilo msimu wa mwaka 2024/2025.


MAKAMU wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakikabidhi kikombe cha ubingwa wa Ligi KuuTanzania Bara (NBCPL) kwa nahodha Yanga SC, Bakari Mwamnyeto.

Hafla ya kukabidhi ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dare es Salaam baada ya mchezo wa mwisho wa ligi hiyo baina ya mabingwa hao na Simba SC ya jijini uliomalizika kwa yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0.

Hafla hiyo iliongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, ambao kwa pamoja walikabidhi kombe hilo.

Akizungumza baada ya tukio hilo, Sabi pamoja na kuwapongeza mabingwa hao na timu nyngine zilivyoshiriki ligi hiyo, alieleza kutiwa zaidi na kasi ya maendeleo a mchezo wa soka nchini hususani ushindani mkubwa unaoshuhudiwa kila msimu.

“Tangu tuanze kudhamini, tumeshuhudia ushindani mkubwa na wa kuvutia kati ya vilabu vyote vinavyoshiriki. Ushindani huu siyo tu umepandisha kiwango cha mchezo, bali pia umetufanya tushuhudie matukio ya kusisimua na burudani ya hali ya juu”, alieleza Sabi.

Aliongeza kuwa hali hiyo inadhihirisha kwamba kila timu inajitahidi kuonesha uwezo wake wa hali ya juu, na hili ni jambo la kufurahisha sana kwetu kama wadhamini.

“Tunapofunga mwaka huu wa mashindano, tunatambua kwamba ushindani ni sehemu muhimu ya maendeleo ya michezo na tunajivunia kuwa sehemu ya safari hii. Napenda kuwahakikishia wapenzi wa mchezo huu kuwa Benki ya NBC itaendelea kuboresha udhamini wa Ligi Kuu ya NBC msimu ujao”, alisema Sabi.

Sabi alitaja jitihada zinazohitaji kipaumbele kuwa ni pamoja na uwezeshaji kwenye michakato ya mafunzo na maendeleo ya wachezaji hususani kwenye programu za vijana, huduma bora za bima husasani ya afya kwa wachezaji na huduma za kibenki mahususi kwa wanamichezo.

Comments

Popular posts from this blog

Airtel Foundation yazindua mpango wa udhamini wa masomo kwa vijana

ZAMECO yakerwa na video ya udhalilishaji mtandaoni

SMZ yawaita vijana kushiriki kilimo