GeSCI kuzindua mpango kuimarisha elimu Tanzania
Katika uzinduzi huo, miongoni mwa wageni watakaohudhuria na kuwasilisha taarifa na mada ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tanzania Bara Prof. Eliamini Sedoyeka, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar Ali Khamis Juma na Khamis Abdulla Said, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar.
Wengine ni Mkurugenzi Taasisi ya Elimu Zanzibar (ZIE), Abdalla Mussa, Dk. Fika Mwakabungu, Mkurugenzi Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Dk. Said Juma, Mkuu wa kitivo cha elimu katika chuo kikuu cha taifa Zanzibar (SUZA) na Khadija Shariff kutoka Milele Zanzibar Foundation.
Wazungumzaji wengine ni Mwanaidi Ali, Mkurugenzi Mtendaji, taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Sr. Grace Mkosamali, RELI TZ nchi /AMUCTA na Mkurugenzi Mtendaji, UWEZO Tanzania, Zaida Mgalla.
Comments
Post a Comment