Simbaya Mkurugenzi mpya UTPC
MUUNGANO wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) umepata Mkurugenzi Mtendaji mpya kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Mkurugenzi wake, Aboubakar Karsan.
Taarifa iliyotolewa na Rais wa UTPC, Deogratius Nsokolo (katikati pichani) kupitia mtandao wake wa Twitter imemtaja Mkurugenzi huyo kuwa ni Keneth Simbaya ambaye aliwahi kuiongoza taasisi hiyo siku za nyuma.
“Nikiwa
Rais wa UTPC nina furaha kutangaza kuwa Union of Tanzania Press Clubs,
(Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania) UTPC, imepata Mkurugenzi
Mtendaji mpya Ndg. Kenneth Simbaya (kulia kwangu), amechukua nafasi ya Abubakar
Karsan (kushoto kwangu) ambaye amestaafu,” alieleza Nsokolo katika taarifa yake
hiyo iliyoambatana na picha akiwa na watendaji wawili hao.
Kwa niaba ya uongozi na wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), inampongeza Ndg. Simbaya kwa kuaminiwa na bodi ya wakurugenzi ya UTPC kushika wadhifa huo lakini pia Ndg. Karsan kwa utumishi wake uliotukuka kwa taasisi hiyo inayowaunganisha wanahabari wa Tanzania kwa lengo la kuimarisha weledi na ustawi wa tasnia ya Habari nchini.
Comments
Post a Comment