Othman aongoza mazishi ya mke wa mwandishi habari Zanzibar
NA
MWANDISHI MAALUM, ZPC
MAKAMU
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Alhaj Othman Masoud
Othman, Septemba 12, 2022 alijumuika na wananchi na viongozi mbali mbali katika
maziko ya mke wa Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima na mwanachama
wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Talib Ussi Hamad, bi. Hafsa
Said Salum.
Maziko
ya bi. Hafsa aliyekua mtumishi wa Baraza la Manispaa Mjini, yalifanyika katika
makaburi ya Kianga baada ya kusaliwa katika msikiti wa Weles, mkoa wa Mjini
Magharibi Unguja.
Akizungumzia
msiba huo uliotokea Septemba 11, mwaka huu, Mwenyekiti wa ZPC, Abdallah
Abdulrahman Mfaume, alitoa pole kwa wafiwa na kuwataka kuwa na subira katika
kipindi hiki kigumu na kumuombea dua marehemu apumzike kwa amani.
Aidha
aliwataka wanachama wa Klabu hiyo na waandishi wa habari Zanzibar kuendeleza
umoja na mshikamano kama waliouonesha katika msiba huo kwa kuwa hupunguza
machungu na kuongeza faraja kwa wafiwa.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala Pema, Amin.
Picha na maelezo
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa marehemu Hafsa Said Salum aliyekua mke wa mwandishi wa habari Talib Ussi Hamad, kabla ya sala maiti iliyofanyika katika msikiti wa Weles, Mjini Unguja.
Comments
Post a Comment