Changamoto sekta ya habari kupatiwa ufumbuzi
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAM
Msemaji Mkuu wa
Serikali Gerson Msigwa alieleza hayo hivi karibuni alipokua akifungua Mkutano
Mkuu Maalum wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),
uliofanyika jijini Dar es salaam.
Alisema
serikali itafanya kazi na waandishi kwa sababu inatambua mchango wa UTPC katika
kunyanyua uwezo wa waandishi wa habari hapa nchini, kuwezesha ofisi za
waandishi wa habari mikoani kufanya kazi, kuchochea maendeleo mikoani na
kupasha habari wananchi waweze kupata uelewa ili kufanya uamuzi sahihi
“Niko tayari
kufanya kazi na UTPC wakati wa shida na raha ninachowaomba msiniangushe mniunge
mkono na mimi nitawaunga mkono waswahili wanasema imani huzaa imani, mimi nina
imani kubwa na UTPC na ninapenda sana umoja huu kwa sababu ninatambua hapa
nilipo ndipo mahali sahihi kwa kuwagusa waandishi wa habari wote bila kujali
maeneo walipo,” alisema.
Alieleza kuwa
moja ya changamoto zinazoikwaza tasnia ya habari ni sheria zinazohitaji
kurekebishwa hivyo alihakikisha dhamira ya serikali ni kutengeneza mazingira
wezeshi kwa vyombo vya habari kufanya kazi katika mazingira yote ambapo alisema
wizara ya habari inajiandaa kuwasilisha bungeni mabadiliko ya sheria ili
wabunge wakiridhia tuendelee na utekelezaji wake.
Wajumbe na waalikwa wakifuatilia hotuba
Msigwa alishauri UTPC kutengeneza mazingira ya kuvutia wawekezaji katika habari kwani hivi sasa vyombo vya habari vingi havilipi mishahara, pia vingi hakuna mikataba ya waandishi wa habari.“Tunatakiwa
tujenge mazingira ambayo watakuja wawekezaji ambao wataona hapo ni mahali pa kuwekeza
ili wakiwekeza walipe mishahara,” alisema.
Alisema Klabu
za waandishi wa habari zinatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya taaluma ya
uandishi wa habari pamoja na kuchangia maendeleo ya mikoa mbalimbali nchini.
“Natoa wito kwa
mamlaka mbali mbali za serikali kutosita kuchangia vilabu vya waandishi wa
habari wa mikoa isiwe ni kuwakumbuka wakati wa matukio pekee bali kwa wakati
wote ikiwemo kipindi ambacho mnatenga bajeti kwa ajili ya kutekeleza shughuli
ambazo mnatambua kuwa zitawashirikisha waandishi wa habari,” alisema.
Awali Rais wa
UTPC, Deogratius Nsokolo, alisema kuna klabu 28, kati ya hizo 26 zipo bara na
mbili zipo Zanzibar lengo likiwa ni kuhakikisha waandishi wanakua na mazingira
wezeshi na salama katika utekelezaji wa majukumu yao.
Alisema lengo lililopo sasa ni kuimarisha Klabu za waandishi wa
habari Dodoma na Dar es Salaam, ikiwezekana makao makuu ya UTPC yahamishiwe
makao makuu ya nchi ili kuwa karibu na viongozi wa serikali na rahisi kufikika
na wadau wa habari.
Aidha katika mkutano huo, wajumbe walipitisha maazimiombali
mbali likiwemo la kuhamisha makao makuu ya taasisi hiyo kutoka Mwanza hadi
Dodoma ili kurahisisha mawasiliano na taasisi mbali mbali za serikali na
binafsi.
Comments
Post a Comment