Dk. Mwinyi ahimiza malezi bora ya watoto, vijana
NA MWANDISHI MAALUM, PEMBA
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameihimiza jamii kuweka mkazo kwenye malezi ya watoto na vijana ili kukuza taifa lenye maadili, nidhamu na kizazi chema chenye kumjua Mwenyezi Mungu.
Dk.
Mwinyi aliyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu
Zanzibar 1445 Hijria yaliyofanyika katika Masjid Munawwara, Mfikiwa mkoa
wa Kusini, Pemba.
Alisema
ni wajibu wa wazazi na walezi kuwasimamia vyema watoto wao na kuwapa elimu ya dini
na dunia ili kuwaepusha na vitendo vya uvunjivu wa amani, tabia mbaya na
vitendo vya udhalilishaji.
Akizungumzia
historia ya tarehe ya Kiislaam, Alhajj Dk. Mwinyi alieleza ilianza mara baada
ya Mtume SAW kuhama Makka na kuhamia Madina ambako utulivu na Amani
ulipatikana na kuwa chanzo cha kuenea uislam dunia nzima.
Alisema
lengo la kuadhimishwa mwaka Mpya wa Kiislam 1445 H ni kuendelea kusisitiza na
kuhimiza amani, ushirikiano na upendo kwenye jamii Katika kutekeleza mambo ya
heri.
Aidha,
aliendelea kuhimiza umoja na mshikamano kwenye jamii ili nchi izidi kupata
neema na baraka kutoka kwa Mola.
Akizungumza
kwenye hafla hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa
Umma na Utawala Bora, Haroun Ali Suleiman, alipongeza ushirikiano uliopo baina
viongozi wa Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba na viongozi wa Chama, katika
kutela Maendeleo ya kisiwa hicho.
Akiwasilisha
mada ya nidhamu ya kodi kwenye kongamano la mwaka mpya wa kiislaam 1445, Sheikh
Said Ahmad aliwataka watumishi wa umma kuutumia vyema muda wao wanapotekeleza majukumu
yao ili kukwepa kuchuma mali za dhulma zinazotokana na utumishi waa hasa kwenye
ibada zao.
Aidha alihimiza
umuhimu wa kulipa Kodi kwa serikali kwa mujibu wa sheria za Kiislam ambapo
Sheikh Izud Alaw kutoka Mombasa Kenya, aliwahimiza waumini wa dini
ya Kiislam juu kuzingatia vyema tarehe za kiislam kwenye mfumo wa maisha yao.
Vile
vile, aliwataka waumini kutofungamana na kufuatilia masuala na muandamo wa
mwenzi na hitilafu za Arafa pekee, bali waangalie mambo mengine muhimu ikiwemo
suala la eda kwa mwanamke alieacha ama kufiliwa na mumewe kwa tarehe zinapoanza
hadi kumalizika kwake.
Akiwasilisha
taarifa ya maadhimisho hayo, Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti, Sheikh Khalid
Mfaume, alisema lengo la maadhimisho hayo ni kuitangaza tarehe ya kiislam na
kuendeleza historia ya dini walioiacha maulamaa na kuahidi Ofisi ya Mufti
inajukimu ya kuendelea kuitangaza na kuishajisha kwa jamii.
Alisema
maadhimisho hayo yanayofikia kilele leo, yalitanguliwa utoaji wa huduma za matibabu
ya macho, dua ya kuliombea taifa, kongamano la wanawake wa Kiislamu
lililohudhuriwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Hajjat Dk. Samia
Suluhu Hassan, maonesho ya biashara yaliyowashirikisha wafanyabiasha wadogo na
wajasiriamali, matembezi ya ZAFA yatakayofanyika kisiwani Pemba yaliyolenga
kuboresha afya pamoja na matembezi ya hiari yatafanyika Unguja.
Comments
Post a Comment