Posts

Showing posts from October, 2024

Kheri ya Siku ya Umoja wa Mataifa (UN)

Image
 

Silaa azindua mnara wa mawasiliano ya simu Makuru

Image
NA SAIDA ISSA, SINGIDA WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, amezindua mnara wa mawasiliano ya simu uliojengwa katika kijiji cha Hika, kata ya Makuru, wilayani Manyoni Singida. Mnara huo uliojengwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa ruzuku inayotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Mwasiliano kwa Wote (UCSAF) ni muendelezo wa juhudi za serikali katika kuboresha upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya vijijini ili kuhamasisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo hayo. Waziri Silaa aliongeza kwa kusema kuwa, dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dk. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kuwa maeneo ya vijijini yanafikiwa na huduma bora za mawasiliano ikiwemo mtandao wa intaneti. "Dhamira yetu ya kimkakati ya kuimarisha muunganisho katika maeneo ya vijijini na sasa tunafanya uboreshaji mkubwa wa minara ya mawasiliano inayofanya kazi kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G/4G", alisema. Kwa upande wake M...

PBZ yashukuru uwepo wa sera, sheria zinazokuza sekta za fedha

Image
  NA MWANDISHI WETU BENKI ya watu wa Zanzibar (PBZ) imezishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa kuweka mazingira wezeshi yanayokuza biashara na kuimarisha sekta za fedha nchini. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi (wa tatu kulia) akipokea zawadi maalum kutoka kwa   Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), Arafat Haji wakati wa  hafla ya ufunguzi wa tawi jipya la benki hiyo wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.  Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mwendeshaji wa benki hiyo, Arafat Haji Ali, wakati wa uzinduzi wa tawi la benki hiyo wilayani Nyamagana, mkoani Mwanza uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi. Arafat alieleza kuwa jitihada zinazofanywa na Rais Dk. Mwinyi na Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, za kubuni miongozo na sera zinazoimarisha ukuaji wa uchumi na kuchochea mafanikio ya taasisi ...

Airtel Foundation yazindua mpango wa udhamini wa masomo kwa vijana

Image
NA MWANDISHI WETU KAMPUNI ya mawasiliano ya Aiirtel Tanzania imezindua mpango wa udhamini wa masomo katika fani za teknolojia kwa vijana wa Afrika wanaosoma katika taasisi ya teknolojia ya india (IIT – Madras) kampasi ya Zanzibar. Uzinduzi huo umefanyika Oktoba 7, 2024 katika kampasi ya chuo hicho Bweleo, wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Dk. Dinesh Balsingh na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Muhamed Mussa. Viongozi wengine ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Omar Kipanga, Balozi wa India nchini Tanzania, Dk. Biswadip Dey, Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Makame Machano Haji na Mkuruaenzi wa IITMZ Prof. Preeti Aghalayam. Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Airtel Africa, Dk. Segun Ogunsanya,   Dk. Dinesh amesema programu hiyo inahusisha wanafunzi wa Afrika walofaulu michipuo ya sayansi na kwamba kila mwak...

Takukuru kuongoza vita dhidi ya rushwa SADC

Image
NA MWANDISHI MAALUM, LUSAKA – ZAMBIA TANZANIA kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imechukua uongozi wa taasisi za mapambano dhidi ya rushwa katika ukanda wa Kusini mwa Afrika (SADC) ikiwa ni mara ya pili kushika nafasi hiyo. Katika hotuba yake ya uzinduzi wa   mkutano wa mwaka wa Wakuu wa Mamlaka za Kupambana na Rushwa kwa nchi za SADC, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Crispin Francis Chalalima (pichani), ambaye pia ni Mwenyekiti mpya wa kamati ya SADC ya kupambana na rushwa (SACC), ametahadharisha kuhusu hatari ya rushwa kwenye utoaji wa misaada wakati wa dharura. Chalamila ameeleza kuwa majanga ya dharura kama vile mlipuko wa magonjwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi yanaweza kufungua milango ya rushwa katika hatua mbalimbali za ugawaji misaada, ikiwa ni pamoja na udanganyifu, ubadhirifu wa mali, na ukiukwaji wa maadili ya ununuzi. “Mchakato wa utoaji misaada upo katika hatari kubwa ya kudhibitiwa na rushwa kwa sababu ya haraka na udharura wa hali ...