UZINDUZI WA RIPOTI YA UTAFITI WA VYOMBO VYA HABARI NA URIPOTI WA UCHAGUZI MKUU 2020, DISEMBA 22, 2021 ZANZIBAR KATIBU Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar, Suleiman Abdallah Salim (kulia), akikata utepe kuzindua ripoti ya utafiti wa vyombo vya habari na uripoti wa uchaguzi mkuu wa 2020, uliofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein uliomo katika jengo la ZURA, Zanzibar. KATIBU Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar, Suleiman Abdullah Salim (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa vyombo vya habari na uripoti wa uchaguzi mkuu wa 2020, Dk. Darius Mukiza, wakionesha ripoti hiyo baada ya kuzinduliwa katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein uliomo katika jengo la ZURA, Zanzibar. Mtafiti Kiongozi, Abadallah Katunzi akitoa maelezo juu ya matokeo ya utafiti vyombo vya habari na uripoti wa uchaguzi mkuu wa 2020 uliofanywa na Shule kuu ya uandishi wa habari ya Chuo Kikuu cha Dar es salam (SJMC) wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo kwa wandishi wa habari na vi...
Popular posts from this blog
Vyombo vya habari vinapaswa kusimamia mshikamano wa Afrika - UAJ
NA MWANDISHI MAALUM, CAIRO MSHAURI wa Baraza Kuu la Usimamizi wa Vyombo vya Habari nchini Misri, Reem Hindi, ameeleza haja ya vyombo vya habari barani Afrika kusimamia msingi wa mshikamano wa Kiafrika ili kustawisha maendeleo ya bara na tasnia ya habari kwa ujumla. Alitoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya 61 yaliyoandaliwa na Umoja wa Waandishi wa Habari wa Afrika (UAJ) kwa kushirikiana na Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari yanayoendelea jijini Cairo, Misri yanayoshirikisha waandishi wa habari kutoka mataifa 20 ya Afrika huku Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ukiwakilishwa na mwanachama wa Klabu ya Waaandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Khairat Haji Ali. Mshauri huyo aliweka wazi dhamira ya nchi hiyo kuunga mkono jitihada za UAJ za kujenga weledi na uhuru wa vyombo vya habari barani Afrika kama miongoni mwa mikakati ya kukuza kasi ya maendeleo na demokrasia. “Kupitia mafunzo, mijadala na kubadilishana uzoefu, vyombo vya habari vitaweza kusaidia nchi za ...
'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS
NA MWANDISHI MAALUM, USWISI WIZARA ya Afya Zanzibar imetunukiwa tuzo ya kimataifa ya ‘ World Summit on the Information Society’ (WSIS) kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mfumo wa matibabu kwa njia ya kadi maalum ya kidijitali ijulikanayo kama ‘ Zanzibar Matibabu Card’ , ambao umewezesha utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi kupitia teknolojia. Hafla ya kukabidhi tuzo hiyo ilifanyika Geneva, Uswisi na kuhudhuriwa na Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania, Jerry Slaa, Balozi wa Tanzania Geneva, Abdallah Possi, pamoja na wajumbe kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar (e-GAZ) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Waziri wa Afya Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui, alisema mpango huo ni uthibitisho wa dhamira ya taifa kutumia teknolojia kuboresha maisha ya wananchi. Alieleza kuwa mfumo huo umeunganisha vituo vyote vya afya vya umma na taarifa za m...

Comments
Post a Comment