NBC yaahidi makubwa ligi kuu Tanzania bara
NA MWANDISHI WETU MDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jana ilikabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya soka ya NBC (NBCPL) kwa timu ya Yanga SC ya jijini Dar es Salaam iliyoibuka bingwa wa kombe hilo msimu wa mwaka 2024/2025. MAKAMU wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakikabidhi kikombe cha ubingwa wa Ligi KuuTanzania Bara (NBCPL) kwa nahodha Yanga SC, Bakari Mwamnyeto. Hafla ya kukabidhi ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dare es Salaam baada ya mchezo wa mwisho wa ligi hiyo baina ya mabingwa hao na Simba SC ya jijini uliomalizika kwa yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0. Hafla hiyo iliongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, ambao kwa pamoja walikabidhi kombe hilo. Akizungumza baada ya tukio hilo, Sabi pamoja na kuwapon...