Posts

NBC yaahidi makubwa ligi kuu Tanzania bara

Image
NA MWANDISHI WETU MDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jana ilikabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya soka ya NBC (NBCPL) kwa timu ya Yanga SC ya jijini Dar es Salaam iliyoibuka bingwa wa kombe hilo msimu wa mwaka 2024/2025. MAKAMU wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakikabidhi kikombe cha ubingwa wa Ligi KuuTanzania Bara (NBCPL) kwa nahodha Yanga SC, Bakari Mwamnyeto. Hafla ya kukabidhi ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dare es Salaam baada ya mchezo wa mwisho wa ligi hiyo baina ya mabingwa hao na Simba SC ya jijini uliomalizika kwa yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0. Hafla hiyo iliongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, ambao kwa pamoja walikabidhi kombe hilo. Akizungumza baada ya tukio hilo, Sabi pamoja na kuwapon...

Viwango bora nyenzo muhimu kukuza masoko kimataifa - Dk. Mwinyi

Image
NA MWANDISHI WETU RAIS wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa usimamizi bora wa viwango vya bidhaa ni nyenzo muhimu kwenye biashara na kukuza masoko kimataifa. Dk. Mwinyi alieleza hayo jana katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla (pichani), alipokuwa akifungua mkutano wa 31 wa Shirika la Viwango Afrika (ARSO), uliofanyika hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa ndege , Zanzibar. Alieleza kuwa serikali za Tanzania zinaelewa jukumu kuu la viwango katika kuwezesha matumizi ya viwango katika biashara kati ya nchi za Afrika ,  kukuza usalama wa watumiaji na kuimarisha ushindani wa viwanda. Aliongeza kuwa kuna umuhimu wa kuendelezwa kwa mikusanyiko na majukwaa kama mkutano huo kwa lengo la kubadilishana uzoefu juu ya kusimamia miongozo ya viwango Afrika  na ku i pongeza ARSO kwa kuendelea kujitolea kuendeleza ubora na kuunganisha miundombinu kila pahala Afrika . Makamu wa Pili wa...

NHIF kutumia wiki ya utumishi wa umma kutoa elimu

Image
  NA SAIDA ISSA, DODOMA KATIKA kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma 2025, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umeweka mkazo katika kuelimisha umma kuhusu magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kuhimiza matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali katika upatikanaji wa huduma zake. Akizungumza kwenye viwanja vya maadhimisho hayo jijini Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa NHIF, James Mlowe (pichani), alisema ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo limeendelea kuwa changamoto kubwa kwa sekta ya afya. “Kwa sasa, zaidi ya asilimia 60 ya gharama zote za matibabu tunayolipa kila mwaka zinahusiana na magonjwa yasiyoambukiza,Kwa mfano, mwaka uliopita NHIF ilitumia takribani shilingi bilioni 700 kwa ajili ya huduma kwa wanachama wake”, alisema. Aidha Mlowe alisisitiza umuhimu wa elimu kwa jamii kuhusu namna ya kujikinga na maradhi hayo, akisema juhudi hizo zitasaidia kupunguza gharama kubwa za matibabu na kuruhusu fedha kuelekezwa katika kubore...

Dk. Samia asema daraja JP Magufuli litafungua fursa usafirishaji kikanda

Image
NA MWANDISHI WETU, MWANZA RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amezindua daraja la JP Magufuli maarufu kama Kigongo - Busisi, mkoani Mwanza. Akizungumza katika hafla hiyo Juni 19, 2025 Rais Samia, alisema daraja hilo linafungua historia mpya katika sekta ya usafiri na usafirishaji kati ya Kigongo na Busisi. Akizungumza na wananchi, alisema aliendeleza ujenzi wa mradi huo uliosisiwa na Rais John Pombe Magufuli kutokana na ahadi yake kwa Watanzania ni kuyaendeleza mambo yote yaliyoachwa na viongozi wa awamu zilizopita na pia kutekeleza mengine mapya. “Leo tunaandika historia mpya kuhakikisha hadithi za kusikitisha zinaondoka juu ya usafisi na usafirishaji”, alisema. Alisema alipokea mradi huo ukiwa umefikia asilimia 25 kwa gharama ya shilingi bilioni 152 ambazo zililipwa kwa wakandarasi, lakini serikali yake imefanikiwa kuendeleza ujenzi wa daraja hilo lenye umuhimu mkubwa kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Alifafanua kuwa daraja hilo limejengwa kwa lengo la kuungan...

Dk. Samia aitaka mahakama kusimamia haki

Image
NA MWANDISHI WETU   RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema matarajio ya Watanzania ni kuona mahakama inasimamia haki. Kauli hiyo alitoa Juni 15, 2025 Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, wakati akimuapisha Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Mcheche Masaju, aliyemteua hivi karibuni. Aidha alisema Watanzania wanatarajia kuona mahakama inaendelea zaidi kutoka ilipo sasa kuanzia majengo, vitendea kazi na mifumo. A idha a lirejea kauli yake aliyoitoa   kati ka kilele cha  siku ya sheria mwezi Februari ,  mwaka huu, kwamba  kazi ya Majaji ni kusimamia haki na  kazi ya kutoa haki  ni ya Mwenyezi Mungu. “Sisi Majaji hatuna kudra wala jaala, kazi yetu ni kusimamia haki kwa misingi tuliyojiwekea, hivyo msisitizo wangu twendeni tukasimamie haki” ,  ames isitiza Dk. Sa m i a. Amesema serikali kwa upande wake itafanya kila linalowezekana kuendelea kufanyia kazi changamoto za mahakama kama alivyoahidi wakati akihutubia bunge k...

ZAMECO yakumbushia sheria mpya ya habari

Image
NA MWANDISHI MAALUM KAMATI ya Wataalamu y a  Vyombo vya Habari Zanzibar (ZAMECO), ime i shauri serikali kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa sheria mpya ya habari ili kuimarisha uhuru wa kujieleza  na uwajibikaji . Akizungumza wa kati  w a kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani upande wa Zanzibar, lililofanyika  Rahaleo  Studio , Mjumbe wa ZAMECO, Salim Said Salim, alisema mchakato huo umechukua muda mrefu   hivyo ipo haja ya kuchukuliwa kwa hatua za makusudi kuukamilisha. “Katika miaka  ya hivi karibuni  tu me shuhudia sheria nyingi zikipitishwa na Baraza la Wawakilishi ila sheria ya habari mchakato wake umekuwa ukienda na kurudi kwa zaidi ya miaka 20 hali inayowafanya wadau wa tasnia ya habari ku jion a wanyonge ”, alisema Salim. BAADHI ya waandishi wa habari na wafdau wa habari wakifuatilia uwaasilishaji wa mada wakati wa kongamano  Aliziomba mamlaka zinazohusika kuendelea kushirikiana na taasisi za kihabari kuhakiki...

2.4trl/- kuing'arisha elimu 2025/26

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA WAZIRI ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeomba kuidhinishiwa shilingi trilioni 2.4 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zake kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Katika kipindi hicho, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa wadau wa elimu na umma kuhusu sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023 pamoja na utekelezaji wa mitaala iliyoboreshwa. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo, alisema Serikali imepanga kutoa mafunzo kwa wathibiti ubora wa shule, walimu wa shule za msingi na sekondari, wakufunzi wa vyuo vya ualimu, maafisa elimu, wakufunzi wa vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi, pamoja na wahadhiri wa vyuo vya elimu ya juu. Alieleza kuwa serikali itakamilisha mapitio ya Sheria ya Elimu Sura ya 353 ili iendane na matakwa ya Sera ya Elimu na Mafunzo 2014 (Toleo la 2023), sambamba na mapitio ya sheria nyingine za taasisi mbalimbali zinazohusika na elimu kama vile Tume ya ...