Posts

'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS

Image
NA MWANDISHI MAALUM, USWISI WIZARA ya Afya Zanzibar imetunukiwa tuzo ya kimataifa ya ‘ World Summit on the Information Society’ (WSIS) kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mfumo wa matibabu kwa njia ya kadi maalum ya kidijitali ijulikanayo kama ‘ Zanzibar Matibabu Card’ , ambao umewezesha utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi kupitia teknolojia. Hafla ya kukabidhi tuzo hiyo ilifanyika Geneva, Uswisi na kuhudhuriwa na Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania, Jerry Slaa, Balozi wa Tanzania Geneva, Abdallah Possi, pamoja na wajumbe kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar (e-GAZ) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Waziri wa Afya Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui,   alisema mpango huo ni uthibitisho wa dhamira ya taifa kutumia teknolojia kuboresha maisha ya wananchi. Alieleza kuwa mfumo huo umeunganisha vituo vyote vya afya vya umma na taarifa za m...

Ufaulu kidato cha sita watahiniwa wa skuli juu

Image
NECTA yazuia matokeo ya watahiniwa 244 NA MWANDISHI WETU KATIBU Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Prof. Said Mohammed (pichani), amesema ufaulu wa watahiniwa wa skuli kwa mwaka 2025 umeongezeka kwa asilimia 0.03 huku ufaulu wa watahiniwa wa kujitegemea ukishuka kwa asilimia 2.64 ukilinganishwa na mwaka jana. Aliyasema hayo wakati akitangaza matokeo ya mitihani ya kidatu cha sita (ACSEE), ualimu daraja la tatu A (GATCE), mtihani wa ualimu daraja la A kozi maalumu (GATSCCE), mtihani wa stashahada ya ualimu wa sekondari (DSEE) iliyofanyika mwezi Mei 2025. Alieleza kuwa hali ya ufaulu wa kijinsia ni sawa kati ya wanawake na wanaume kwa asilimia 93.34 na kubainisha kuwa walioshindwa kufanya mitihani kwa watahiniwa wa skuli ni 68 sawa na asilimia 0.05. Aidha alifafanua kuwa watahiniwa wa skuli waliofaulu ni 125,779 sawa na asilimia 99.95 ya watahiniwa waliofanya mitihani, ukilinganisha na watahiniwa 103,252 sawa na asilimia 99.92 ya watahiniwa wa skuli kwa mwaka jana. “Mwak...

NBC yaahidi makubwa ligi kuu Tanzania bara

Image
NA MWANDISHI WETU MDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jana ilikabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya soka ya NBC (NBCPL) kwa timu ya Yanga SC ya jijini Dar es Salaam iliyoibuka bingwa wa kombe hilo msimu wa mwaka 2024/2025. MAKAMU wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakikabidhi kikombe cha ubingwa wa Ligi KuuTanzania Bara (NBCPL) kwa nahodha Yanga SC, Bakari Mwamnyeto. Hafla ya kukabidhi ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dare es Salaam baada ya mchezo wa mwisho wa ligi hiyo baina ya mabingwa hao na Simba SC ya jijini uliomalizika kwa yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0. Hafla hiyo iliongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, ambao kwa pamoja walikabidhi kombe hilo. Akizungumza baada ya tukio hilo, Sabi pamoja na kuwapon...

Viwango bora nyenzo muhimu kukuza masoko kimataifa - Dk. Mwinyi

Image
NA MWANDISHI WETU RAIS wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameeleza kuwa usimamizi bora wa viwango vya bidhaa ni nyenzo muhimu kwenye biashara na kukuza masoko kimataifa. Dk. Mwinyi alieleza hayo jana katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla (pichani), alipokuwa akifungua mkutano wa 31 wa Shirika la Viwango Afrika (ARSO), uliofanyika hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa ndege , Zanzibar. Alieleza kuwa serikali za Tanzania zinaelewa jukumu kuu la viwango katika kuwezesha matumizi ya viwango katika biashara kati ya nchi za Afrika ,  kukuza usalama wa watumiaji na kuimarisha ushindani wa viwanda. Aliongeza kuwa kuna umuhimu wa kuendelezwa kwa mikusanyiko na majukwaa kama mkutano huo kwa lengo la kubadilishana uzoefu juu ya kusimamia miongozo ya viwango Afrika  na ku i pongeza ARSO kwa kuendelea kujitolea kuendeleza ubora na kuunganisha miundombinu kila pahala Afrika . Makamu wa Pili wa...

NHIF kutumia wiki ya utumishi wa umma kutoa elimu

Image
  NA SAIDA ISSA, DODOMA KATIKA kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma 2025, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umeweka mkazo katika kuelimisha umma kuhusu magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kuhimiza matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali katika upatikanaji wa huduma zake. Akizungumza kwenye viwanja vya maadhimisho hayo jijini Dodoma, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa NHIF, James Mlowe (pichani), alisema ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo limeendelea kuwa changamoto kubwa kwa sekta ya afya. “Kwa sasa, zaidi ya asilimia 60 ya gharama zote za matibabu tunayolipa kila mwaka zinahusiana na magonjwa yasiyoambukiza,Kwa mfano, mwaka uliopita NHIF ilitumia takribani shilingi bilioni 700 kwa ajili ya huduma kwa wanachama wake”, alisema. Aidha Mlowe alisisitiza umuhimu wa elimu kwa jamii kuhusu namna ya kujikinga na maradhi hayo, akisema juhudi hizo zitasaidia kupunguza gharama kubwa za matibabu na kuruhusu fedha kuelekezwa katika kubore...

Dk. Samia asema daraja JP Magufuli litafungua fursa usafirishaji kikanda

Image
NA MWANDISHI WETU, MWANZA RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amezindua daraja la JP Magufuli maarufu kama Kigongo - Busisi, mkoani Mwanza. Akizungumza katika hafla hiyo Juni 19, 2025 Rais Samia, alisema daraja hilo linafungua historia mpya katika sekta ya usafiri na usafirishaji kati ya Kigongo na Busisi. Akizungumza na wananchi, alisema aliendeleza ujenzi wa mradi huo uliosisiwa na Rais John Pombe Magufuli kutokana na ahadi yake kwa Watanzania ni kuyaendeleza mambo yote yaliyoachwa na viongozi wa awamu zilizopita na pia kutekeleza mengine mapya. “Leo tunaandika historia mpya kuhakikisha hadithi za kusikitisha zinaondoka juu ya usafisi na usafirishaji”, alisema. Alisema alipokea mradi huo ukiwa umefikia asilimia 25 kwa gharama ya shilingi bilioni 152 ambazo zililipwa kwa wakandarasi, lakini serikali yake imefanikiwa kuendeleza ujenzi wa daraja hilo lenye umuhimu mkubwa kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Alifafanua kuwa daraja hilo limejengwa kwa lengo la kuungan...

Dk. Samia aitaka mahakama kusimamia haki

Image
NA MWANDISHI WETU   RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema matarajio ya Watanzania ni kuona mahakama inasimamia haki. Kauli hiyo alitoa Juni 15, 2025 Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, wakati akimuapisha Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Mcheche Masaju, aliyemteua hivi karibuni. Aidha alisema Watanzania wanatarajia kuona mahakama inaendelea zaidi kutoka ilipo sasa kuanzia majengo, vitendea kazi na mifumo. A idha a lirejea kauli yake aliyoitoa   kati ka kilele cha  siku ya sheria mwezi Februari ,  mwaka huu, kwamba  kazi ya Majaji ni kusimamia haki na  kazi ya kutoa haki  ni ya Mwenyezi Mungu. “Sisi Majaji hatuna kudra wala jaala, kazi yetu ni kusimamia haki kwa misingi tuliyojiwekea, hivyo msisitizo wangu twendeni tukasimamie haki” ,  ames isitiza Dk. Sa m i a. Amesema serikali kwa upande wake itafanya kila linalowezekana kuendelea kufanyia kazi changamoto za mahakama kama alivyoahidi wakati akihutubia bunge k...