UZINDUZI WA MPANGO WA UWEZESHAJI MADEREVA BODABODA, BAJAJI ULIOFANYIKA KATIKA HOTELI YA UBUNGO PLAZA DAR ES SALAM
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi, Biashara ndogo na za Kati Benki ya NMB, Filbert Mponzi, akitoa maelezo juu ya mpango wa uwezeshaji madereva bodaboda na bajaji wakati wa uzinduzi wa mpango huo hafla hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Ubungo Plaza, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akifurahia jambo pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (kushoto). Kulia ni Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi, Biashara ndogo na za Kati Benki ya Nmb, Filbert Mponzi.
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akionesha funguo za bodboda kabla ya kumkabidhi mmoja ya madereva wakati wa hafla ya Uzinduzi wa mpango wa uwezeshaji wa fursa za mikopo kwa madereva Bajaji na Bodaboda ujulikanayo kama 'NMB MASTABODA – MILIKI CHOMBO, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Ubungo Plaza, Jijini Dar Es Salaam.
PICHA KWA HISANI YA OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, URATIBU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU.
Comments
Post a Comment