NA MWANDISHI MAALUM, WKUMM WIZARA ya Kilimo Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo imeeleza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali kupitia taasisi zake kustawisha sekta ya kilimo na ufugaji. Waziri wa wizara hiyo, Shamata Shaame Khamis alieleza hayo baada ya kushuhudia utiaji saini ya makubaliano ya ushirikiano na kiutendaji kati ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Zanzibar (ZALIRI) na taasisi ya Friedrich Loeffler Institut (FLI) ya nchini Ujerumani. Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ZARILI, Talib Saleh Suleiman alitia saini kwa niaba ya taasisi hiyo na kwa upande wa FLI, Mkurugenzi wa Institute of International Animal/One Health, Prof. Sascha Knauf aliiwakilisha taasisi yake. Waziri Shamata alieleza kuwa serikali ya Ujerumani imekuwa na ushirikiano wa karibu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika mipango yake ya maendeleo. Alifahamisha kuwa utiaji saini huo utaongeza ufanisi na wataalamu wa utafiti wa masuala ya mifugo lakini
Comments
Post a Comment