Waandishi watakiwa kuelimisha jamii chanjo ya kipindupindu
NA KHADIJA KHAMIS, MAELEZO
Akifungua mafunzo
kwa waandishi wa habari kuhusu chanjo hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya
Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Zanzibar, Dkt. Abdallah Ali
Suleiman (pichani), amesema lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu kwa jamii ili
kuondokana na dhana potofu zinazotokana na chanjo hiyo
Amesema chanjo hiyo
haina madhara kwa binadamu na inatolewa kwa ajili ya kuikinga jamii na maradhi
ya mripuko hivyo ameitaka kuondoa shaka hiyo.
Ameeleza kuwa chanjo
hiyo inatarajiwa kutolewa kwa mwezi ujao katika shehia mbali mbali za Unguja na
Pemba kwa maeneo ambayo huathirika sana kila unapotokea mripuko wa maradhi
hayo.
Nae Afisa Afya
ya Jamii, Fauza Mohamed Abdulkadir, amesema chanjo hiyo inatarajiwa
kutolewa kwa watu wenye umri wa mwaka mmoja na kuendelea na wagonjwa wenye
maradhi sugu yasiyoambukizwa yakiwemo presha sukari na mengineyo.
“Chanjo hiyo haitopaswa kupewa wagonjwa mahatuti na mama
wajawazito na watoto chini ya mwaka mmoja,” alifahamisha Afisa huyo.
Kwa upande wake
Mratibu wa chanjo kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Vendelin Simon,
amesema kuwa chanjo iko salama tayari imeshatolewa katika nchi mbalimbali
na haijaleta madhara yoyote kwa waliotumia ambayo ni dawa ya kunywa sio
sindano hivyo ameisihi jamii kuwa na mwamko wa kushiriki kupata chanjo hiyo.
Zoezi la utoaji wa chanjo ya kipindupindu linatarajiwa kufikia
zaidi ya watu 300,000 katika Wilaya tisa za Unguja na Pembazenye jumla ya
shehia 58 ikiwa na lengo la kutoa kinga kwa wananchi katika kipindi cha
miaka mitatu hadi mitano.
PICHA
WADAU wa Afya, Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Afya wakiwa katika picha ya pamoja na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbali mbali baada ya mafunzo ya siku moja kuhusu kampeni ya chanjo ya kipindupindu yaliyofanyika katika ukumbi wa ZSSF, Kariakoo Zanzibar.(PICHA NA FAUZIA MUSSA, MAELEZO – ZANZIBAR).
Comments
Post a Comment