Wanachama Yanga SC wakubali mabadiliko
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAM
WANACHAMA wa Klabu ya Yanga ya jijini Dar es salam wamekubali rasmi
kuingia katika mfumo wa mabadiliko ya uendeshaji na mabadiliko ya katiba kwenye
mkutano mkuu uliofanyika Juni 27, mwaka huu.
Mwenyekiti wa
Yanga, Dk. Mshindo Msolla akiongoza mkutano huo, aliwauliza wanachama kuhusu
kuafiki mabadiliko hayo mara baada ya kutambulisha kamati iliyosimamia mchakato
wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji.
Wajumbe 1,170 ambao
walijiandikisha katika Mkutano Mkuu uliofanyika katika ukumbi wa DYCC, jijini Dar
es Salaam walipitisha mabailiko hayo kwa kura za ndio.
Baada ya Dk. Msolla
kuwauliza wanachama wanaoafiki mabadiliko hayo na ukumbi mzima ukanyoosha
mikono akiwamo, Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Jakaya Kikwete, aliyekuwa mgeni
rasmi huku baadhi yao wakipiga kelele kuwa wote wanaafiki.
Baada ya hatua
hiyo, Dk. Msolla aliwakabidhi vyeti wajumbe wa kamati hiyo na kisha akarejea
tena kwa wanachama kuwauliza wasioafaki na hakuna mkono ulionyooshwa.
Sehemu ya
mabadiliko kwa klabu ya Yanga ni kuifanya timu hiyo kuwa kampuni huku klabu
ikimiliki hisa aslimia 51 na wawekezaji wakimiliki hisa asilimia 49.
Comments
Post a Comment