Marekebisho sheria huduma za habari Januari
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
Alisema katika bunge litakaloanza Januari mwakani, wizara hiyo inatarajia kupeleka marekebisho ya sheria hiyo ili ifanyiwe marekebisho katika baadhi ya vifungu, hali ambayo itakuza uhuru wa habari.
Nape alieleza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, itashirikiana na vyombo vya habari na kwamba itawezesha kuweka mazingira mazuri na kuondosha vikwazo kwa wanahabri.
Aliongeza kuwa sekta ya habari inaendelea vizuri na uhuru wa habari umeimarika, kwani hakuna hakuna mwandishi aliyepotea, hakuna anayefinywa, ambapo Rais Samia amefanya mabadiliko makubwa katika kukuza uhuru wa habari nchini.
Katika Waziri Nape alitoa maagizo matano kwa wadau hao kuwa sekta ya habari ni muhimu hivyo wizara itaendelea kushirikiana na kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili zitafanyiwa kazi.
Alisema mwaka unafuata nguvu zaidi zitawekwa kwa ajili ya maslahi ya waandishi wa habari ikiwemo masuala ya bima, ambapo alimtolea mfano mwandishi wa TBC aliyefariki baada ya kupanda mlima Kilimanjaro Kapembe ambae ameacha familia itaangaliwaje.
Sambamba na kuvihimiza vyombo vya habari kufanya kazi kwa kuzingatia miiko, maadili na utamaduni wa nchi na wajibu wa kulinda rasilimali za nchi ili zisitumike vibaya na kusababisha mvurugano.
Alisema kongamano hilo litakuwa endelevu na litafanyika kila mwishoni mwa mwaka ambalo litaboreshwa na liwe la Kongamano la kimataifa naaendeleo ya sekta ya Habari.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Jim Yonazi alisema jukumu la Wizara wakati wa matumizi ya Tehama kuleta mabadiliko ya kiuchumi kupitia Teknolojia ya Mawasiliano nchini.
Comments
Post a Comment