Tabia kuvalia njuga changamoto za waandishi wa habari
NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Tabia Mauld Mwita, ameahidi kuvalia njuga changamoto zinazowakabili waandishi wa habari wa vyombo vya binafsi ili wanufaike na kazi wanazozifanya kwenye vyombo hivyo.
Ameeleza hayo
Disemba 26, 2022 wakati akifungua mkutano mkuu maalum wa Klabu ya waandishi wa
habari Zanzibar (ZPC), uliofanyika katika ukumbi wa Uhuru uliopo katika viwanja
vya kufurahishia watoto Kariakoo Zanzibar.
Ameeleza kuwa
anatambua changamoto zinazowakabili waandishi na watendaji wa vyombo vya habari
hasa vya binafsi hivyo atafanya ziara za kushitukiza ili kujionea na kuona
hatua za kuchukua kustawisha hali za wafanyakazi wa vyombo hivyo.
Swala la
wafanyakazi wa vyombo binafsi kutokua na mikataba nalifahamu lakini pia
nafahamu mambo mengi ndio maana nmepanga kufanya ziara za kushitukiza ili
nikajionee mwenyewe na nitachukua hatua kwa kushirikiana na taasisi au wizara
nyengine,” amesema Tabia.
Waziri Tabia akifungua mkutano
Aidha waziri huyo amepongeza
kazi kubwa zinazofanywa na vyombo vya habari na kuvitaka kuendelea kufanya
hivyo kwa kuzingatia misingi ya taaluma, sheria na maadili huku akiahidi kwamba
serikali itaendelea kuweka mazingira ya kisera na kisheria kwa lengo la
kuiimarisha kada ya uandishi wa habari.
Akizungumzia mchakato
wa upatikanaji wa sheria mpya ya habari, Waziri huyo ameeleza kuwa unaendelea
vyema na kwamba mswada wa sherisa hiyo unatariwa kupelekwa katika baraza la
wawakilishi katika vikao vya awali ya mwaka ujao wa 2023.
Akimkaribisha Waziri
Tabia, Mwenyekiti wa ZPC, Abdallah Mfaume, alimuomba kusimamia na kuzipatia
ufumbuzi changamoto zinazowakabili wandishi wa habari wa vyombo vya habari
binafsi ili wafanye kazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha amezungumzia
haja ya kurejeshwa kwa posho la mazingira magumu walilokua wakilipwa waandishi
wa habari wanaofanya kazi katika vyombo vya serikali kwani kazi wanazofanya
zinalingana na watumishi wengine wanaolipwa posho hilo.
Awali akitoa
maelezo ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa ZPC, Mwinyimvua Nzukwi, ameeleza mkutano
huo ni maalum kwa ajili ya kupitia na kuridhia mipango na maazimio ya mabadiliko
ya kiutendaji naliyoanza kutekelezwa na Muungano wa Klabu za Waaandishi wa
habari Tanzania (UTPC).
Waziri Tabia (katikati walioketi) katika picha ya pamoja baadhi ya wakufunzi wa ZPC
Ameeleza kuwa katika utekelezaji wa majukumu yake, zpc na utpc imeamua kuchukua hatua za kuimarisha utendaji chini ya kauli mbiy ya ‘kutoka ubora kwenda ukubwa’ inayolenga kuziimarisha taasisi hizo.Katika mkutano huo
pamoja na kuchangia taarifa zilizowasilishwa walipendekeza na kuthibitisha
majina ya wajumbe wa bodi, wajumbe wa kamati ndogo ndogo, kufanya mabadiliko ya
katiba na kuridhia kwa kauli moja maazimio yaliyofikiwa katika mkutano mkuu
maalum wa utpc uliofanyika jijini Dar es salam Disemba 7, 2022.
Comments
Post a Comment