Balozi Mpanda ahimiza ubunifu uhifadhi wa mazingira
JUVIEKA, wadau wapanda mikoko 2,540 Mtopwani NA MWANDISHI WETU JUMLA ya miche ya miti ya mikoko 2,540 imepandwa katika eneo la Mdodo madema, Shehia ya Mto wa pwani mkoa wa Kaskazini Unguja ili kutunza mazingira ya eneo hilo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mratibu wa zoezi hilo ambaye ni kiongozi wa Jumuiya ya Vijana ya Uhifadhi wa Mazingira, Mbarouk Maalum, alieleza kuwa zoezi hilo lililofanyika jumapili iliyopita lilihudhuriwa na wanaharakati wa mazingira 117 kutoka taasisi na makundi mbali mbali ya jamii. Aliongeza kuwa miongoni mwa washiriki hao ni vikundi vitano vya wanufaika wa mpango wa MKUBA, wanachama na viongozi wa mabaraza ya vijana ya Shehia za Mtowapwani na Chutama, wawakilishi taasisi za JUVIEKA, UNA, ZAFELA pamoja na Sheha wa Shehia hiyo na wananchi wake. Aidha maalum alieleza kuwa shughuli hiyo pia ilihudhuriwa na Balozi wa mazingira kutoka ofisi ya rais, Muungano na Mazingira ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Khadija Yussuph Mpanda ambaye pia ni mion
Comments
Post a Comment