Dk. Samia akemea viongozi wachonganishi
NA MWANDISHI MAALUM, MUNDULI
Rais Samia amesema hayo, wakati akizungumza katika Kumbukumbu ya Miaka 40 ya kifo cha Hayati Edward Moringe Sokoine huku akiwasisitiza viongozi kuiga mfano wa Sokoine kwani alikemea jambo hilo kwa maneno na vitendo.
Rais Samia
amesema Hayati Sokoine alitumia
utashi wake wa
hali ya juu kuimarisha mahusiano
kati ya serikali
na jamii aliyoiongoza na
kuiwakilisha vyema jamii ya Wamaasai.
Aidha amewataka viongozi
wa sasa na wajao kutambua
kuwa uamuzi ukifanyika ndani ya serikali
ni wajibu wao kuutekeleza kama ulivyo hata ikibidi wao wawe mfano kwa wengine
kama Hayati Sokoine alivyofanya.
Kuhusu umuhimu
wa elimu kama
ulivyopewa kipaumbele na
Hayati Sokoine, Rais Samia ametoa
wito kwa wazazi kutumia vyema fursa ya miundombinu bora ya Elimu inayojengwa na
serikali kuwapeleka watoto shule.
Aidha Rais Samia
ametoa wito kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora,
kuendelea kutunza kumbukumbu
za viongozi wa kitaifa na kuhakikisha habari zao zinawafikia vijana
wengi zaidi kupitia njia za kisasa.
Rais Samia
ametumia fursa hiyo
pia kutoa pole
kwa waathiriwa wote
wa mafuriko na kuahidi
kuwa serikali itaendelea
kufanya kila linalowezekana kuepusha madhara
zaidi na kuwataka
pia wananchi kusikiliza
maelekezo ya tahadhari
zinazotolewa.
Pia Rais
Samia amesema baada
ya mvua hizo
na hali ya kawaida
kurejea, Serikali itafanya uchunguzi wa kina kubaini sababu za mafuriko
hayo ili kuepusha madhara makubwa kwa siku zijazo.
Comments
Post a Comment