Posts

Showing posts from November, 2024

Maafisa Habari Z'bar watakiwa kuongeza kasi ya uwajibikaji

Image
NA MWANDISHI WETU WAZIRI wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo, Tabia Maulid Mwita, amewataka Maofisa Habari na Mawasiliano wa wizara na taasisi za serikali kutekeleza majukumu yao vyema na kutoa taarifa za utendaji wa serikali kwa wananchi. Waziri Tabia alieeleza hayo jana katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil, Kikwajuni, mjini Unguja wakati wa uzinduzi  wa Jumuiya ya Maafisa Habari na Mawasiliano Zanzibar (ZICCO) na kusema maafisa hao na watu binafsi wana jukumu la kuhakikisha kuwa wananchi  wanapata habari za taasisi zao  kwa wakati na usahihi. "Kuna miradi mingi ya maendeleo inafanyika katika taasisi zenu lakini wananchi hawaelewi kutokana na taasisi hizo kukaa kimya bila kuijulisha jamii", alisema Waziri Tabia. Alifafanua kuwa kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu 18 (1 na 2) kinatoa uhuru kwa kila mtu kuwa na haki ya kupokea na kutoa habari na kinaonesha haki ya raia kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio yanayofanyika nchini na duni...

Dk. Samia ataka waumini kutumia nyumba za ibada kujijenga kiimani

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amewataka waumini wa madhehebu mbali mbali nchini kuhakikisha wanatumia nyumba za ibada kwa ajili ya kujijenga kiimani badala ya kugeuza kuwa maeneo ya kufanya vurugu na kusababisha uvunjifu wa amani. Dk. Samia aliwataka wazazi hususani wanawake kuhakikisha wanatenga muda kwa ajili ya malezi ya watoto wao kwani kwa sasa watoto wengi wamekuwa wakiharibika kutokana na kutokuwa naa malezi mema. Alisema hayo jana mjini Morogoro wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi wa msikiti wa Alghaith inayosimamiwa na taasisi ya The Islamic Foundation. Alisema nyumba hizo za ibara ni vyema zikatumika kuunganisha kamba ya waumini na sio kukata kamba hiyo inayounganishwa na Mungu halafu wakajiita ni viongozi wa dini huku wakisababisha mifarakano kwa waumini wao na kuwataka kutofikia huko na kwamba binadamu huwa wanatofautiana. Aidha alizungumzia suala la malezi ya watoto aliwataka wazazi hususani akima mama kuhakikisha wanatenga muda wa kutos...

Polisi Zanzibar yatoa tamko siku 16 kupinga GBV

Image
  TAMKO LA KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR, CP HAMAD KHAMIS HAMAD KUADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WASICHANA Ndugu Wananchi, Leo tunajiunga na dunia nzima kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili Dhidi ya Wanawake na Wasichana. Haya ni maadhimisho muhimu ambayo hutufanya kutafakari kwa kina madhara ya ukatili wa kijinsia katika jamii zetu na kuchukua hatua madhubuti za kulinda haki za wanawake na wasichana, ambao ni nguzo muhimu za maendeleo ya taifa letu. Kaulimbiu ya mwaka huu inatukumbusha dhamira yetu ya pamoja ya kuimarisha juhudi za kuzuia ukatili wa kijinsia na kuhakikisha usawa wa kijinsia kwa kila mmoja. Ni ukweli usiopingika kuwa ukatili dhidi ya wanawake na wasichana sio tu ukiukwaji wa haki za binadamu, bali pia ni kikwazo kikubwa katika kufikia maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi. Ndugu Wananchi, Jeshi la Polisi Zanzibar linasimama mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa kesi za ukatili wa kijinsia zinashughulikiwa kwa haraka na haki ...

Programu ya IMASA kuwanufaisha wananchi, wajasiriamali wadogo – Ayoub

Image
NA MWANDISHI MAALUM MKUU wa Mkoa wa Kusini Unguja, Ayoub Mohammed Mahmoud, amesema programu ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) ina manufaa makubwa katika kuimarisha uchumi wananchi wa Zanzibar  wenye kipato cha chini na kujikimboa na umasikini. MKUU wa Mkoa wa Kusini Unguja, Ayoub Mohammed Mahmoud, akifungua programu ya Imarisha Uchumi na Mama Samia (IMASA) mkoani humo katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu. Program u  hiyo inasimamiwa na Baraza la Uwezeshaji Tanzania (NEEC) kwa kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) . Kauli hiyo aliitoa wakati akifungua mkutano wa programu hiyo ambayo imezinduliwa kwa mara ya kwanza Zanzibar  kwa wajasirimali wa mkoa wa kusini Unguja hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohammed Shein, Tunguu Zanzibar. Alisema kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakipata uwezeshaji kwa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara, afya, Maji na miundombinu nyengine lakini dhamira ya Dk. Samia na Dk. H...

Dk. Samia aweka maneno ushindi wa Stars AFCON

Image
MUDA mchache baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya timu ya taifa ya tanzania ‘TAifa Stars’ na  Guinea , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amewapongeza wachezaji, viongozi na watanzania kwa timu hiyo kuibuka na ushindi wa goli 1 – 0. Kupitia kupitia mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter), Dk. Samia alieleza;    “Tukiwa katika majonzi na kazi ikiendelea katika kuwatafuta ndugu zetu ambao tunaamini bado wapo hai kufuatia kuporomoka kwa jengo eneo la Kariakoo, ninawapongeza vijana wetu Taifa Stars kwa ushindi na kufuzu kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025”. Dk. Samia aliongeza kwa kusema; “Mmeandika historia kwa Taifa letu, ikiwa ni mara yetu ya nne kufikia mafanikio haya makubwa katika kipindi cha zaidi ya miaka arobaini”. Alliongeza kwa kusema; “Hongera kwa kazi nzuri nyote tuliowapa dhamana kusimama na vijana wetu kukamilisha jukumu hili katika Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Benchi ...

Nsokolo ajiuzulu urais UTPC

Image
NA MWANDISHI WETU RAIS wa Muungano wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),   Deogratius Nsokolo (pichani) amejiuzulu wadhifa huo kufuatia kupata uteuzi wa kutumikia taasisi nyengine ya kisiasa hivi karibuni. Nsokolo aliyekuwa akikamilisha kipindi cha pili cha uongozi wake katika nafasi hiyo, alifikia uamuzi huo Novemba 10, mwaka huu na kwamba Makamu wake, Pendo Mwakyembe atakaimu nafasi ya Rais hadi utakapofanyika uchaguzi mkuu wa taasisi hiyo inayoundwa na klabu 28 za waandishi wa habari nchini. Taarifa iliyotolewa kwa viongozi wa klabu za wanahabari Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC, Keneth Simbaya hivi karibuni na, ilithibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa kiongozi huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari Kigoma na mwandishi wa kituo cha televisheni ya ITV mkoani humo. Kaimu Rais wa UTPC, Pendo Mwakyembe “Napenda kuwafahamisha kuwa tumepokea rasmi barua ya kujiuzulu kwa Rais wa UTPC, Deogratius Nsokolo tarehe 10 Novemba, 2024 baada ya kupata ut...

Upigaji kura ‘Samia Kalamu Awards’ waanza rasmi

Image
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM ZOEZI la upigaji kura kwa washiriki wa tuzo Samia Kalamu Awards, limeanza Novemba 11 na litakamilika Novemba 20 , mwaka huu. Tuzo hizo zimeandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Kwa  mujibu  wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, upigaji kura utahusisha  wananchi kwa asilimia 60 ya  matokeo kwa kuwa ndio walaji wa maudhui na asilimia 40 ya alama za vigezo vya kitaaluma zitatolewa na jopo la majaji. Watakaopigiwa  kura ni wanahabari na vyombo  vilivyokidhi vigezo  vya kitaaluma  vya uandishi wa habari za maendeleo ambapo makala 1,131 ziliwasilishwa  kutoka  mikoa yote ya Tanzania bara na  Zanzibar kuwania tuzo hizo. Aidha chambuzi za  kitaaluma 85 zilizokidhi vigezo ambazo zimewekwa tovuti ya Samia Awards na mitandao ya kijamii pia zitapigiwa kura. Taarifa hiyo imesema tuzo hizo zinalenga kuhamasisha, ...

ZAMECO yakerwa na video ya udhalilishaji mtandaoni

Image
NA MWANDISHI WETU KAMATI ya Wataalamu wa Masuala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) inayoundwa na taasisi za kihabari na wadau wa habari imelaani video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayoonesha wasichana wawili waliorekodiwa na kuulizwa maswali yasiyo na maadili, kuvunja heshima na kukiuka haki za binaadamu. Taarifa iliyotolewa na taasisi hizo na kutiwa saini kwa pamoja na mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Abdallah Mfaume na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA ZNZ), Dk. Mzuri Issa, ilieleza kuwa tukio hili limeibua hisia kali kwa wadau wa habari, watetezi wa haki za binaadamu najamii kwa ujumla. Ilielezwa kuwa tukio hilo pia limeibua maswali yasiyo na majibu miongoni mwa wanahabari kuhusu maadili, haki za binadamu, na misingi ya uhuru wa vyombo vya habari. “Hivyo basi ZAMECO inasisitiza kuwa vitendo vya udhalilishaji kwa watoto wa kike na jamii ni ukiukwaji wa haki za binaadamu, maadili ya uandishi wa habari na kuvuruga ...