Posts

Showing posts from May, 2025

ZAMECO yakumbushia sheria mpya ya habari

Image
NA MWANDISHI MAALUM KAMATI ya Wataalamu y a  Vyombo vya Habari Zanzibar (ZAMECO), ime i shauri serikali kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa sheria mpya ya habari ili kuimarisha uhuru wa kujieleza  na uwajibikaji . Akizungumza wa kati  w a kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani upande wa Zanzibar, lililofanyika  Rahaleo  Studio , Mjumbe wa ZAMECO, Salim Said Salim, alisema mchakato huo umechukua muda mrefu   hivyo ipo haja ya kuchukuliwa kwa hatua za makusudi kuukamilisha. “Katika miaka  ya hivi karibuni  tu me shuhudia sheria nyingi zikipitishwa na Baraza la Wawakilishi ila sheria ya habari mchakato wake umekuwa ukienda na kurudi kwa zaidi ya miaka 20 hali inayowafanya wadau wa tasnia ya habari ku jion a wanyonge ”, alisema Salim. BAADHI ya waandishi wa habari na wafdau wa habari wakifuatilia uwaasilishaji wa mada wakati wa kongamano  Aliziomba mamlaka zinazohusika kuendelea kushirikiana na taasisi za kihabari kuhakiki...

2.4trl/- kuing'arisha elimu 2025/26

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA WAZIRI ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeomba kuidhinishiwa shilingi trilioni 2.4 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zake kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Katika kipindi hicho, Serikali itaendelea kutoa elimu kwa wadau wa elimu na umma kuhusu sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023 pamoja na utekelezaji wa mitaala iliyoboreshwa. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo, alisema Serikali imepanga kutoa mafunzo kwa wathibiti ubora wa shule, walimu wa shule za msingi na sekondari, wakufunzi wa vyuo vya ualimu, maafisa elimu, wakufunzi wa vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi, pamoja na wahadhiri wa vyuo vya elimu ya juu. Alieleza kuwa serikali itakamilisha mapitio ya Sheria ya Elimu Sura ya 353 ili iendane na matakwa ya Sera ya Elimu na Mafunzo 2014 (Toleo la 2023), sambamba na mapitio ya sheria nyingine za taasisi mbalimbali zinazohusika na elimu kama vile Tume ya ...

Naibu Waziri azindua miradi ya kiuchumi ya watu wenye ulemavu

Image
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Ummy Nderiananga amezindua miradi ya kiuchumi ya shirika la Strategic Alternative Learning Technique (SALT), inayohudumia vijana wenye changamoto za ufahamu. Nderiananga alifanya uzinduzi huo jijini Dar es Salaam kwa miradi ambayo ni pamoja na SALT Special Supermarket, Mgahawa na Bekari itakayohudumiwa na vijana wenye ulemavu wa ufahamu huku akisema jumla ya vijana na Watoto 83 wamepatiwa mafunzo ya namna ya kutoa huduma kwa wananchi hatua itakayowasaidia kujipatia kipato chao na kuchangia maendeleo ya Taifa. Aidha aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu, kujiwezesha kiuchumi na kusaidia mashirika yanayoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu. “Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali yake ya Awamu ya Sita i...

Mbunge Ikupa ahimiza wenye ulemavu kulinda amani

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA MBUNGE wa Viti Maalum Stella Ikupa amewahimiza watu wenye ulemavu kuendelea kuenzi hali ya amani na utulivu vilivyopo nchini na kuwataka kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Akizungumza wakati akifungua kongamano la watu wenye ulemavu lililoandaliwa na Ikupa Trust Fund alisema watu wenye ulemavu ni moja ya makundi ya Mwanzo yatakayopata shida kama machafuko yatatokea kwa sababu yoyote ile . "Ninawaomba ndugu zangu,tunapoelekea katika uchaguzi mkuu, tuendelee kuiombea nchi yetu amani iendelee kudumu, tusikubali kuwa sehemu ya jambo lolote ambalo ni kinyume ,maana machafuko yakitokea nchini ,sisi walemavu ndio waathirka wa kwanza, tukifiatiwa na akina mama na watoto, tumuombe Mwenyezi Mungu uchaguzi uwe wa amani, tukatae wanahamasisha virugu”, alisema Ikupa. Aidha Ikupa alitumia fursa hiyo kuipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mambo men...

Msiwanyanyapae watoto wenye ulemavu – DC Hamid

Image
MKUU wa wilaya ya Mjini, Hamid Seif Said (pichani), amewataka wazazi kutowaficha na kuwanyanyapaa watoto wenye ulemavu badala yake wawajumuishe kwenye shughuli mbali mbali ili wapatiwe haki zao na kushiriki katika maendeleo. kizungumza wakati wa Tamasha la Furaha Jumuishi kwa Watoto Wenye ulemavu, lililofanyika Aprili 5, 2025 katika viwanja vya kufurahishia watoto Kariakoo Zanzibar, amesema kuwafungia ndani kunawanyima fursa ya kuendeleza vipaji vyao na kupata maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesema watoto wenye ulemavu wana haki sawa na watoto wengine hivyo kuna ulazima wa jamii kutambua umuhimu wa kundi hilo kuunnga mkono juhudi zinazochukuliwa na serikali kuwapatia haki zao. MKUU wa Wilaya ya Mjini, Hamid Seif Said (katikati),  Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu Zanzibar, Mhandisi Ussi Khamis Debe na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Salma Saadati Haji, w akikata keki  kuzindua Tamasha la Furaha Jumuishi kwa Watoto wenye Ulemavu wa wilaya ya Mjini. “Serikal...

NBC yaahidi kumuunga mkono Rais Samia kuimarisha ustawi wa wafanyakazi

Image
NA MWANDISHI WETU BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kubuni huduma mahususi za kibenki kwa ajili ya makundi mbali mbali ya watumishi wa umma na sekta binafsi ili kuchochea kasi ya ukuaji uchumi kupitia rasilimali watu. Hatua hiyo pia ni kuunga mkono jitihada za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania inayoongozwa na rais, dk. Samia Suluhu hassan inayolenga kuimarisha maisha ya wafanyakazi na kukuza ujumuishaji wa kifedha. Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa benki hiyo, Godwin Semunyu, alieleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa Habari kupongeza hatua ya serikali kupitia Rais Dk. Samia kutangaza ya nyongeza ya kima cha chini cha mshahara kutoka shilingi 370,000 hadi shilingi 500,000 sawa na ongezeko la asilimia 35.1. Dk. Samia alitangaza uamuzi huo kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Bombadia, mkoani Singida hivi karibuni ambapo benki hiyo ilikuwa mi...

ZiBi, OER waiweka Zanzibar kwenye ramani ya uwekezaji duniani

Image
NA MWANDISHI WETU JARIDA la Biashara na Uwekezaji Zanzibar (Zanzibar Investment and Business Insights  - ZiBi) limeweka historia baada ya kutambulika rasmi kama mshirika wa kimataifa wa  jarida   maarufu la biashara katika n chi za Ghuba   la Oman Economic Review (OER) . Taarifa iliyotolewa na waandaaji wa jarida hilo, ilieleza kuwa hatua iliyofikiwa ni kubwa kwa sekta binafsi ya Zanzibar na uthibitisho wa uwezo wa taasisi za ndani kushindana na kushirikiana kimataifa. Katika kilele cha O man E conomic R eview  Business Summit 2025 iliyofanyika Aprili  30, 2025  mjini Muscat, ZiBi ilialikwa kama Mgeni Maalum na kutangazwa kuwa ni Msirika wa habari kwa Zanzibar (Media Partner – Zanzibar)  huku iki wakilishwa na Mjumbe wa Bodi ya ZiBI, Masoud Salim . “Wa kati  w a hafla hiyo, ZiBi ilitunukiwa tuzo maalum ya kutambuliwa kama mshirika wa habari kutoka Zanzibar  ikia ni i shara ya heshima kubwa kwa mchango wake katika kukuza uhusiano wa kiuch...