Toeni taarifa za madhila mnayofanyiwa kazini – Simbaya

NA MWANDISHI WETU MKURUGENZI Mtendaji wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya (wa pili kushoto aliyeshikana mikono na Katibu wa KGPC - Mwajabu Hoza) amewahimiza waandishi wa Habari kutoa taarifa za madhila wanayofanyiwa wanapokua kazini ili hatua zichukuliwe. Simbaya alitoa wito huo mkoani Kigoma alipokua akizingumza na waandishi wa habari wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani humo (KGPC), alipofika kujitambulisha kwa wanachama na kueleza mipango ya utekelezaji wa mpango wa mkakati wa UTPC wenye kaulimbiu ya ‘Kutoka kwenye ubora kwenda kwenye ukubwa (Moving from good to great). Mkurugenzi huyo aliyembatana na Ofisa Programu, Mafunzo, Utafiti na Machapisho, Victor Maleko, alisema hatua hiyo itapunguza vitendo hivyo vinavyopunguza uhuru wa vyombo vya habari nchini. MKURUGENZI Mtendaji wa Muungano wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya (wa pili kushoto) akieleza jambo kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa...